Sandro Rosell
Rais
wa klabu ya Barcelona, Sandro Rosell, amejiuzulu kufuatia madai ya
utumizi mabaya ya fedha wakati klabu hiyo ilipomsajili nyota wa Brazil,
Neymar mwaka uliopita.
Rosell,
amesema madai yanadhamiria kumharibia sifa na kuwa sio ya kweli lakini
amehisi hadhi ya heshima ya klabu hiyo itahujumiwa ikiwa ataendelea
kuhudumu kama rais wa klabu hiyo.
“The
Board of Directors is a team. And this team leads a project that has
brought the Club great success. I don’t want unfair attacks to
negatively affect their management or the image of the Club. This is why
I think my time here has come to an end. Now, in accordance with the
Club’s Statutes, I have presented my irrevocable resignation of the
presidency of FC Barcelona to the Board of Directors,” alisema Sandro.
Mapema
wiki hii, gazeti moja nchini Uhispania liliandika kuwa klabu hiyo
ilitumia Euro milioni 40 zaidi kuliko ilivyotangazwa kumsajili mchezaji
huyo kutoka Brazil. Ripoti zinasema kuwa baba yake na Neymar na mawakala
wengine waliohusika na mkataba huo walilipwa kiasi fulani cha pesa
ambacho hakikutangazwa.
0 comments:
Post a Comment